Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Diwani aliefukuzwa CHADEMA Arusha arudi CUF

DSCN5390Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF na mchumi mahiri duniani, Prof Ibrahimu Lipumba akimtambulisha Ndg John Bayo ambae aliwahi kuwa Diwani wa Kata ya Elerai Jijini Arusha kabla ya kuvuliwa uananchama wa chama hicho na Kamati Kuu kufuatia kuingia muafaka na CCM akiwa na madiwani wengine 4, muafaka ambao haukuafikiwa na chama kuhusiana na sakata la uchaguzi wa meya wa Manispaa ya Arusha.

Hata hivyo, kuhamia kwake CUF sio rekodi mpya katika maisha yake ya kisiasa kwasababu ameelezwa kuwa miongoni mwa waasisi wa chama hicho mkoani hapa na alishiriki kutafuta wadhamini wakati wa usajili wa chama hicho. kwa hiyo ni kama anarudi alikowahi kuwa zamani.

CUF leo walikuwa na mkutano wenye sura ya kitaifa katika viwanja vya Levolosi Jijini Arusha kwa maana kwamba viongozi karibu wote wa kitaifa walihudhuria mkutano huo sambamba na msafara wa wanachama zaidi ya 300 kutoka Dar es Salaam. Miongoni mwa viongozi waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Prof Lipumba, Katibu Mkuu Maalim Seif S hamad ambae pia ni Makamu wa Rais Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.

Wengine ni Naibu Katibu Mkuu bara, Julius Mtatiro, Makamu Mwenyekiti, Machano Ally na viongozi wengine wengi wakiwemo mawaziri wa chama hicho katika SUK Zanzibar.

Swala la madiwani wa Arusha, zinazodaiwa kuwa vurugu za kisiasa, udini katika siasa, utawala mbovu wa CCM na Chadema kwa ujumla ni miongoni mwa masuala yaliyozungumzwa katika mkutano huo.

Kwa upande mwingine chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) wao walikuwa na Mkutano wao katika Kata ya Sombetini ambapo alikuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Lema alihutubia na kuuza kadi za chama kwa mamia ya watu waliojitokeza katika mkutano huo. Lema amekata rufaa kuvuliwa ubunge na rufaa hiyo inatarajiwa kusikilizwa Jumanne ijayo, Oktoba 2, 2012.

DSCN5378Meza ya viongozi wakuu wa chama cha wananchi CUF

DSCN5394Sehemu ya Jukwaa Kuu la viongozi waalikwa

DSCN5406Hoyce Temu akirukaruka ishara ya mchakamchaka kusalimia wapenzi wa CUF.

DSCN5409Naibu Katibu Mkuu Bara, Julius Mtatiro akizungumza katika kkutano huo leo

DSCN5421Katibu Mkuu wa CUF na Makamu wa Rais Zanzibar, Maalim Seif akizungumza

DSCN5437Mwenyekiti wa chama hicho Prof Lipumba akifafanua jambo katika mkutano wa leo Arusha

DSCN5424Sehemu ya wananchi waliokuwa wakisikiliza hotuba za viongozi. Kuna taarifa za kuaminika zinaeleza kuwa miongoni mwa waliohudhuria mkutano huu kuna watu zaidi ya 300 waliotoka Dar es Salaam, morogoro na Tanga wakitumia usafiri wa mabasi madogo 10 yenye uwezo wa kubeba watu 30 kila moja. Nao walikuja kushuhudia uzinduzi wa mchakamchaka wa CUF kuelekea 2015 kwa upande wa Arusha.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO