Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Majaji wa Mahakama ya Haki za Binadamu ya Afrika kuapishwa leo Jijini Arusha

MAHAKAMA ya Haki za Binadamu ya Afrika leo (Jumatatu) inatarajia kuwaapisha majaji wapya wawili, Ben Kioko, kutoka Kenya na El Hadji Guissé kutoka Senegal.

Mbali ya kuapishwa huko, kutafanyika uchaguzi wa rais wa mahakama hiyo pamoja na na makamu wake baada ya rais wa sasa Jaji, Gerard Niyungeko kutoka Burundi na makamu wake Sophia Akuffo wa Ghana kumaliza kipindi chao cha miaka miwili ya uongozi.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na ofisa habari wa mahakama hiyo, Jean-Pierre Uwanone, hafla hiyo itafanyika kwenye makao makuu ya mahakama hiyo yaliyopo jijini hapa.

Alisema kuwa majaji hao wanaoapishwa waliteuliwa wakati wa mkutano wa 19 wa wakuu wa nchi za Afrika uliokaa Julai 16, mwaka huu, ambapo majaji hao wanatarajiwa kutumikia mahakama hiyo kwa kipindi cha miaka sita.

na Grace Macha, Arusha

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO