Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Valerie Msoka ndie mrithi wa Ananilea Nkya

Chama cha Wanahabari Wanawake (TAMWA) kimepata Mkurugenzi Mtendaji mpya ambae anachukua nafasi ya Ananilea Nkya aliemaliza muda wake baada ya kutumikia taasisi hiyo kwa miaka kumi na moja.

Mkurugenzi huyo mpya, Valerie Msoka ambae ni miongoni mwa wanahabari wanawake 12 waanzilishi wa TAMWA amefanya kazi za kutukuka katika ngazi ya kitaifa, kikanda na kimataifa.

Valirie alikabidhiwa ofisi jana Alhamis Septemba 27, 2012 katika sherehe fupi iliyofanyika ofisi za TAMWA zilizopo Sinza Mori, Dar es Salaam.

Valerie aliwahi kufanya kazi Redio Tanzania, BBC idhaa ya Kiswahili na Kiingereza kabla ya kujiunga na umoja wa mataifa.

Valerie ana shahada ya Uzamili katika fani ya uandishi wa habari kimataifa (M>A International Journalism) kutoka Chuo Kikuu cha City nchini Uingereza, na amefanya kazi maeneo yenye vita kama Sudan, Iraq, Rwanda, Congo na Burundi.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO