Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Ufafanuzi Juu Ya Barabara Itakayopita Serengeti

Wizara ya Maliasili na Utalii imefafanua kuwa barabara ambayo nchi ya Ujerumani imependekeza kuwa ingependa kuifadhili ni ile ambayo inaanzia Mto wa Mbu mkoani Arusha kwenda Mkoani Mara kwa kupitia nje ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti upande wa Kusini. Barabara iliyopendekezwa haitapita kabisa ndani ya Hifadhi hiyo.

Ufafanuzi huu umetolewa baada ya magazeti mawili ya hapa nchini yanayotolewa kwa lugha ya Kiingereza (toleo la tarehe 4 Septemba) kuandika kuhusiana na barabara hiyo bila kuweka wazi kuhusu ramani ya barabara ambayo Naibu Balozi wa Ujerumani aliitaja hivi karibuni alipomtembelea Waziri wa Maliasili na Utalii

Aidha, gazeti mojawapo kati ya hayo mawili, toleo la tarehe 5 Septemba 2012 liliandika tahariri iliyoonyesha kuwa barabara iliyopendekezwa itapita ndani ya Hifadhi ya Serengeti upande wa Kaskazini, hiyo siyo kweli maana Naibu Balozi hakusema hivyo.

Mazungumzo kuhusu suala hili la barabara ya Serengeti yalifanyika tarehe tarehe 3 Agosti 2012 wakati Naibu Balozi wa Ujerumani wa hapa nchini Bw. Hans Koeppel alipomtembelea Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe Khamis Kagasheki na kumwambia kuwa nchi yake iko tayari kufadhili upembuzi yakinifu na ujenzi wa barabara itakayozunguka Hifadhi ya Taifa ya Serengeti upande wa Kusini kama nchi hiyo itaombwa kufanya hivyo. Waziri Kagasheki alilipokea pendekezo hilo na kuahidi kulipeleka kwa Waziri wa Ujenzi Mhe Dkt Magufuli.

George Matiko

MSEMAJIWIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Tarehe 8 Septemba 2012

Simu: +255 784 46804

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO