Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

News Update: Mkutano wa CHADEMA uliokuwa ufanyike Jijini Arusha leo Umeahirishwa, Rufaa ya Lema hatihati kusikilizwa kesho

Taarifa za kuaminika zimemnukuu Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Arusha, Bw Amani Golugwa akitangaza kuahirishwa kwa mkutano mkubwa wa kisiasa uliokuwa umepangwa kufanyika leo katika viwanja vya NMC, vilivyoko eneo la Unga Lt Jijini Arusha.

Kwa mujibu wa chanzo cha taarifa, uamuzi wa kuahirisha mkutano huu unafuatia kushindikana kuutumia uwanja huo baada ya kile kinachoelezwa kuwa hujuma za baadhi ya watendaji wa Serikali.

Inaelezwa kuwa kitendo cha Mkurugenzi wa Manispaa kuamua ghafla kuendesha zoezi

la kuandaa eneo hilo kwa ajili ya shughuli za wamachinga wa Jijini hapa ndicho kimesababisha Mkutano huo usiweze kufanyika kwa siku ya leo.

Awali ilielezwa kuwa, kwa siku ya jana hadi usiku kulikuwa na pilika pilika nyingi katika uwanja huo kuzungushia mabomba ya kuweka uzio na kusambaza vifusi kwenye mashimo yaliyo viwanjani hapo, hali iliyotafsiriwa na baadhi ya watu kuwa inaweza kuwa ni mkakati wa kuhujumu mkutano huo usifanyike hapo.

Haijaweza kufahamika mara moja kama zoezi hilo la kubadili matumizi ya uwanja huo lina baraka za baraza la Madiwani ama ulikuwa ni uamuzi wa Mkurugenzi mwenyewe.

Rufaa ya Lema

Katika hatua nyingine, kuna taarifa za wasiwasi kuhusiana na kama rufaa ya Lema kupinga kuvuliwa ubunge wake inaweza kusikilizwa kesho Septemba 20, kama ilivyokuwa imepangwa hapo awali.

Upande wa mrufani (Lema) uliandika barua kwa Msajili wa Mahakama kuomba shauri hilo lisogezwe mbele kutokana na msimba uliompata mmoja wa mawakili wa upande wa walalamikaji, Mh Tundu Lissu aliefiwa na baba yake mzazi wikendi iliyopita!

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO