Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

TASWIRA: Mkutano wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi ya Kusini mwa Afrika (SADC TROIKA)

Rais Jakaya Kikwete leo (jana) alikuwa na mkutano wa dharura wa wakuu wa nchi kutoka Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (TROIKA) ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Rais Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa asasi hiyo, ameitisha mkutano huo kwa ajili ya kuzungumzia mgogoro wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa jana kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, mkutano huo wa siku moja ulifanyika jijini Dar es Salaam kuanzia jana, Septemba 4, 2012.

Nchi ambazo ni wajumbe wa asasi hiyo ni Msumbiji ambayo ni Mwenyekiti wa sasa wa SADC, Afrika Kusini iliyokuwa Mwenyekiti wa asasi hiyo kabla yaTanzania na Namibia ambayo ni Makamu Mwenyekiti wa asasi hiyo ya Troika.

Wakuu wa nchi hizo waliwasili nchini kuanzia juzi kwa ajili ya kuhudhuria mkutano huo.

Zifuatazo ni picha toka ofisi kuu, Ikulu za mkutano huo.

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz25aP512l9

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO