Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAONI YA WANANCHI: MKUTANO WA MNYIKA MTANDAONI KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA YA HIFADHI ZA JAMII KWA HATI YA DHARURA KUREJESHA FAO LA KUJITOA

image

Katika mkutano wa leo, pamoja na mambo mengine napendekeza maoni yatolewe kuhusu masuala yafuatayo:

Mosi, kuhusu taarifa ya Serikali kuwa marekebisho kuhusu kusitisha fao la kujitoa yamefanyika ili kutimiza lengo na madhumuni ya Hifadhi ya Jamii ambayo ni kuhakikisha kuwa Mwanachama anapostaafu anapata mafao bora yatayomwezesha kumudu hali ya maisha uzeeni.

Pili, kwamba mchakato wa marekebisho hayo ulihusisha wadau kwa kuzingatia utatu yaani wawakilishi kutoka Vyama vya Wafanyakazi, Chama cha Waajiri na Serikali

Tatu, kuwa mchakato unaendelea wa kuandaliwa kwa miongozo na kanuni za mafao ambazo lengo lake ni kuboresha maslahi ya wanachama kwa kutambua tofauti za ajira, tofauti za mazingira ya kazi, tofauti za sababu za ukomo wa ajira na umuhimu wa mwanachama kunufaika na michango yake wakati angali katika ajira.

Nne, juu ya uamuzi wa kusitisha maombi mapya ya kujitoa kwa kipindi cha miezi sita kufuatia kuanza kutumika kwa sheria mpaka pale miongozo itakapotolewa na elimu kwa wadau kuandaliwa.

Tano, maoni mahsusi ya kuingizwa kwenye Muswada Binafsi wa Sheria kwa mujibu wa Kanuni ya 81 (1), Taarifa ya Muswada huo kwa mujibu wa Kanuni ya 81 (2), hati ya kuwasilisha muswada kwa dharura na hoja ya kutengua masharti kuhusu muda wa utangazaji wa Miswada ya Sheria kwa mujibu wa Kanuni ya 81 (5) ya Kanuni za Kudumu za Bunge (Toleo la Mwaka 2007).

GONGA HAPA KUSOMA MUONGOZO NA MAREJESHO WA MAONI HALISI

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO