Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MUHIMU!! MUHIMU!! TANGAZO KWA WANAFUNZI WOTE WA CHUO CHA UHASIBU ARUSHA

demo.slide6gk-is-118

CHUO CHA UHASIBU ARUSHA


Kutokana na Chuo kufungwa, Baraza la Uongozi wa Chuo katika kikao chake cha dharura cha tarehe 03 Mei 2013 kimeagiza wanafunzi wote kuanzia ngazi ya Cheti mpaka Stashahada ya Uzamili kuzingatia yafuatayo:


1. Kila Mwanafunzi anatakiwa kutuma maombi mapya ya kujiunga na Chuo.


2. Barua ya maombi hayo ipitishwe kwa Mkuu wa Wilaya anapoishi mwanafunzi. Kwa mwanafunzi wa Stashahada ya Uzamili ya Uhasibu barua yake ya maombi ipitie kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali.

3. Katika maombi hayo mwanafunzi anaagizwa kueleza namna alivyoshiriki katika vurugu za tarehe 24 Aprili 2013.

4. Mwanafunzi awe amekamilisha malipo ya ada iliyobaki wakati anatuma maombi yake.


5. Mwisho wa maombi ni tarehe 16 Mei 2013.


Tangazo halisi hili hapa


Maombi yapelekwe kwa anwani ifuatayo:


Mkuu wa Chuo,
Chuo cha Uhasibu Arusha
S. L. P. 2798
Arusha.


08 Mei 2013


DSC06585
Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO