Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Rufaa ya Lema yaahirishwa tena…

RUFAA ya kupinga kuvuliwa ubunge wa aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), imesikilizwa leo na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa, wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande, na kisha kuahirishwa hadi siku ambayo itatangazwa baadae

SAM_4599Viwanja vya Mahakama Kuu Arusha vikiwa vimefurika watu wakati wa mjadala wa rufaa ya Lema. Hapa kama picha inavyoonesha, rufaa imekwisha ahirishwa na wananchi hawa wanaondoka maeneo hayo..

DSCN5552Baadhi ya wananchi waliokusanyika nje ya ofisi za Chadema Mkoa wa Arusha, eneo la Ngarenaro wakimsikiliza Mh Godbless Lema haonekeni pichani mara baada ya kutoka Mahakamani kusikiliza shauri lake kupinga kuvuliwa ubunge. Picha hii ni taswira nusu ya kwanza ya watu

DSCN5541Mh Lema akizungumza kuagana na wananchi waliokuwa nae  Mahakamani, mbele ya ofisi za chama hicho muda mfupi uliopita

DSCN5551Hii ni nusu nyingine ya taswira halizi za wananchi waliofika ofisini hapo

DSCN5537

DSCN5534

kutoka MahakamaniShamrashamra barabarani wakitoka Mahakamani hii leo

Wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiandamana kutokea mahakamani,ambapo rufaa ya aliekua Mbunge wa Chadema jijini Arusha Bw. Godbless Lema, ilisikilizwa na kusogezwa mbele. Wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiandamana kutokea mahakamani,ambapo rufaa ya aliekua Mbunge wa Chadema jijini Arusha Bw. Godbless Lema, baada ya kusogezwa mbele. Wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)wakiongozana na aliekua Mbunge wa Chadema jijini Arusha Bw. Godbless Lema Mbunge kutokea mahakamani ambapo rufaa yake ilisikilizwa. Aliekua Mbunge wa Chadema jijini Arusha Bw. Godbless Lema akionekana juu ya gari pamoja naWafuasi wa Chama hicho wakitokea mahakamani. Wafuasi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakibembea juu ya gari la Mbunge. Gari lilipopambwa kwa nakshi za M4C likifuata msafara wa Aliekua Mbunge wa Chadema jijini Arusha Bw. Godbless Lemawakitokea mahakamani. Picha nne za mwisho na Audiface Jackson Blog!

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO