Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Breaking News: Mlipuko Mkubwa Umeelezwa Kutokea Kanisani, eneo la Olasiti Jijini Arusha

Taarifa ambazo Blog hii imezipata hivi punde zinaeleza kuwa mlipuko mkubwa umetokea Jijini Arusha katika Kanisa Katoliki lililopo eneo la Olasiti.

Inaelezwa kuwa leo kulikuwa na Ibada ya kuzindua Parokia ya Mt Joseph Olasiti ambapo Balozi wa Papa alikuwa miongoni mwa wageni.

Mlipuko huo unahisiwa kutokana nakinachohisiwa kuwa bomu la kurusha kwa mkono ambalo linadaiwa kurushwa na mtu aliyepita jirani na Kanisa hilo.

Tunaendelea kufuatilia taarifa zaidi kujua hali ilivyojiri na tutakujuza hapa hapa muda mfupi ujao…DSCN2226

DSCN2228Ulinzi ukiimarishwa eneo ulipotokea mlipuko huo na kujeruhi makumi ya waumini

DSCN2236

DSCN2267Mkuu wa Mkoa wa Arusha, magesa Mulongo akipata maelezo toka kwa padri wa kanisa la Mt Joseph Olasiti ambapo mlipuko huo umetokea..

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 maoni:

Anonymous said...

kweli ni uhasama huu.......ndio tuseme visa vya Zanzibar ndio vimefika Arusha? Mungu wape nguvu majeruhi wote. Wewe shetani hauwezi shinda.

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO