Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Diwani wa CHADEMA atimiza ahadi ya kujenga kisima cha maji kwa shule ya msingi Jijini Arusha

Picha zifuatazo zinaonesha matukio tofauti katika ziara ya Diwani wa Kata ya Levolosi iliyopo Jijini Arusha, Mh Ephata Nanyaro (CHADEMA), akikagua maendeleo ya kazi ya uchimbaji kisima kwa ajili ya wananchi wa kata yake, hususani wananfunzi na walimu wa Shule ya Msingi Levolosi.

Ziara hiyo ya ukaguzi ilifanyika shuleni hapo siku ya Oktoba 10, 2012.

SAM_5387Diwani wa Kata ya Levolosi (mwenye nguo nyeusi), Ephata nanyaro pamoja na walimu wa Shule ya Msingi Levolosi wakiangalia namna ya uchimbaji wa kisima hicho alichoahidi wakati wa kampeni zake kuwania nafasi ya kuongoza Kata hiyo.

SAM_5374Mh Nanyaro (kulia) akipata maelezo kutoka kwa mtaalamu wa uchimbaji visima ambae alieleza kuwa kisima hicho wamechimba urefu wa mita 63 kwenda chini.

SAM_5367Mtaalamu akielekeza matabaka tofauti ya udongo waliyokutana nayo wakati wa uchimbaji, matabaka ambayo huwasaidia kujua upatikanaji wa maji katika eneo husika.

SAM_5376

SAM_5357

SAM_5366

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 maoni:

Anonymous said...

inapendeza kuona vijana wenye umri mdogo wakifanya mambo makubwa na yenye maendeleo...asilimia kubwa ya viongozi wetu wana umri mkubwa na wamekaa madarakani muda mrefu lakini hakuna chchote wanachokifanya...hongera sana kijana Diwani kwa kazi nzuri unayoifanya..natumai ni maandalizi mazuri kwa ajili ya uongozi wa juu zaidi ktk taifa letu...

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO