Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Jackson Wilson Makala: SIJASIMAMISHWA BAVICHA, CHADEMA IS MY LIFE STYLE!

 

KAMANDA mpambanaji wa Chadema kutokea Babati Jackson Wilson Makala (pichani juu), amekanusha vikali habari zilizosambaa kwa watu tofauti waliokaribu nae zikimhusisha na sekeseke la kuwavua uanachama wa Baraza la Vijana Chadema ambalo limeleta sintofahamu dhidi yake baada ya  gazeti moja la kila siku kumuandika jana kuwa nae ni miongoni mwa vijana waliosimamishwa kwa muda katika baraza hilo (BAVICHA kwa makosa tofauti ya utovu wa nidhamu.

Katika mawasiliano yake na Blog hii, jioni ya leo Makala ameeleza kusikitishwa na upotoshwaji huo ambao anadai kwa kiasi fulani umemuathiri kwa kuzingatia uaminifu ambao amejijengea miongoni mwa viongozi na wanachama wengine wa chama chake, na watanzania kwa ujumla.

“Napenda kutoa maelezo mafupi kuhusu habari iliyoandikwa na gazeti la jana (jina linahifadhiwa). Mimi Jackson Wilson Makala sijasimamishwa uanachama na Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA) kama ilivyotaarifiwa na gazeti hilo. Nimewasiliana na Mhariri wa habari wa gazeti… na amekiri kuwa walifanya makosa makubwa katika habari ile.

Ukweli ni kwamba Baraza la vijana CHADEMA taifa jana mchana limetoa tamko la ufafanuzi kuhusu maamuzi ya Kamati Tendaji ya BAVICHA na hakuna popote lilipotaja jina la Jackson Wilson Makala kuwa amesimamishwa uanachama.
NAPENDA KUKANUSHA KUWA HABARI ZILE NI ZA UONGO NA HAZINA UKWELI WOWOTE!
CHADEMA IS MY LIFE STYLE!”
anamaliza kutoa ufafanuzi wake.

Sehemu ya habari hiyo iliyoleta utata kwa kumtaja Bw Makala kimakosa kuwa miongoni mwa vijana waliosimamishwa Chadema ilisomeka hivi ikirejea kikao cha Kamati Tendaji iliyoketi Januari 5, 2013 “Kikao hicho pia kilichukua uamuzi mgumu wa kuwasimamisha uanachama kwa muda wa mwaka mmoja, Gwakisa Mwakisando (Mbeya), Wilson Makala (Babati) na Joseph Kasambala (Mbeya)”

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO