Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

SHIRIKA LA NSSF LAKABIDHIWA RASMI JENGO LAKE JIPYA JIJINI ARUSHA LILILOGHARIMU BILIONI 29 TOKA KWA MKANDARASI

DSCN7402Wataalamu wa ujenzi pamoja na wawakilishi wa Shirika la NSSF katika picha ya pamoja mara baada ya makabidhiano ya Jengo kubwa na la kisasa la shirika hilo lililojengwa Jijini Arusha, barabara ya Old Moshi. Jengo hilo lenye jumla ya ghorofa 15, mbili zikiwa chini (basement) kwa ajili ya maegesho ya magari linaelezwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni 28.75 na limejengwa kwa muda wa miaka miwili.

Kamapuni ya China Jiangchang Engineering Co. Ltd (CRJE) ndiyo imekabidhi mradi huo ramsi hii leo baada ya kukamilika ujenzi wake uliowashirikisha pia wakandarasi wadogo 6 wa ndani.

Jiji la Arusha limepata muonekano mpya kwa kuongezewa jengo refu, kubwa na la kisasa kwa shughuli za kiosifi na biashara. NSSF nao wanategemea kuhamishia offisi zao kwa kanda hii katika jengo hili, halikadhalika huduma za kibenki zitapatikana hapo.

DSCN7392Sehemu ya mbele ya jengo, upande wa kushoto

DSCN7393Jengo jipya la Shirika la Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (NSSF) lililoko Jijini Arusha, Barabara ya Old Moshi. Jengo hilo limekabidhiwa leo kwa shirika hilo toka kwa mkandarasi kutoka China ambae alishirikiana na wakandarasi wengine wa ndani.

DSCN7396

DSCN7353Mkadiriaji na msimamizi wa gaharama za mradi, QS Komba akifafanua jambo kwa mwakilishi wa NSSF, Eng. Mattaka wakati wa ukaguzi wa jengo hilo leo kabla ya makabidhiano ramsi.

DSCN7354Timu ikifanya ukaguzi eneo la kuegesha magari ndani ya jengo hilo

DSCN7376Mbunifu wa jengo, mwakilishi wa NSSF, Injinia Mshauri pamoja na injinia mkaazi wakipata chakula cha mchana kilichoandaliwa maalumu kwa ajili yao na wataalalmu wengine walioshiriki katika ujenzi wa mradi huo, katika hoteli ya kitalii ya Kibo Palace ya Jijini Arusha

DSCN7380Wakandarasi wa kichina pamoja na mkadiriaji majenzi wa mradi, QS Komba wakiwa katika maakuli

DSCN7404Mkadiriaji majenzi wa mradi huo, QS Komba na wataalamu wengine waliofanikisha mradi huo, pamoja na mwakilishi wa NSSF wakiangalia picha za jengo hilo walizopiga hii leo Jijini Arusha

DSCN7345Architect Dudley Mawalla kutoka MD Consultancy Ltd ya Jijini Dar es Salaam (aliyekunja mikono), ambae ndiye mbunifu wa jengo hilo la NSSF Jijini Arusha katika mkutano wa makabidhiano  ya mradi baada ya kukamilika kwa matumizi hii leo.

DSCN7350Wataalamu waliofanikisha design na michoro ya jengo hilo, wakandarasi wa kichina pamoja na mwakilishi wa NSSF, Eng Mataaka wakibadilishana mawazo mara baada ya kikao cha makabidhiano ya mradi kutoka kwa mkandarasi kwenda kwa NSSF.

DSCN7361Injinia Mattaka (katikati) kutoka NSSF akipata ufafanuzi kutoka kwa wataalamu wa usalama wa jengo hilo namna ambavyo mitambo ya kiusalama imefungwa na inavyofanya kazi.

DSCN7405

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO