Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Polisi Arusha wanasa shehena ya mirungi ikisafirishwa

Askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha wakiharibu madawa ya kulevya aina ya mirungi iliyokamatwa leo asubuhi eneo la Engikareti Wilayani Longido, Arusha baada ya msaada mkubwa wa taarifa kutoka kwa raia wema. Gari iliyokamatwa na mirungi hiyo ni aina ya Mitsubish Canter, lenye namba za usajili T 306 BUN gari ambalo pia lina kesi nyingine mahakamani  kutokana na kukamatwa Machi 16, mwaka 2012 likiwa pia na shehena ya mirungi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Liberatus Sabas akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kukamata madawa hayo aina ya mirungi iliyokuwa imehifadhiwa kwenye viroba zaidi ya 200 viliyokuwa vinasafirishwa kuingia nchini kutokea nchini Kenya.

Kamanda  Sabas, alisema hadi sasa wanawashikilia watu wanne waliosafisha mirungi hiyo. Aliwataja waliokamatwa kuwa ni wakazi wa Oldonyosambu Arumeru, Joel Lukumay, Mussa Mollel, mkazi wa Sombetini Arusha, Rahimu Gilla na mkazi wa Ngaramtoni, Ibrahimu Katambweli.

Gharama halisi za mirungi hiyo haikuweza kufahamika mara moja lakini kwa uzoefu inakadiriwa kufikia Sh milioni 30.

DSCN7217Madawa ya kulevya aina ya ‘mirungi’ yakiwa yamemwagwa chini katika uwanja wa Kituo Kikuu cha Polisi Arusha, kutoka kwenye mifuko ilimokuwa imehifadhiwa baada ya gari lililokuwa likiyasafirisha kunaswa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha mapema asubuhi ya leo.

DSCN7219

DSCN7220

Gari iliyokamatwa na mzigo huo ukiwa umechanganywa na piki piki

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO