Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Sheria ya kusimamia vyombo vya habari yaja

Nembo-ya-Taifa

Serikali inapenda kuufahamisha umma wa Watanzania kwamba mchakato wa maandalizi ya kutungwa kwa Sheria ya Kusimamia Vyombo vya Habari (Media Services Bill) upo katika ngazi za juu  Serikalini.

Mswada huo unatarajiwa  kuwasilishwa  Bungeni wakati wowote baada ya kupitishwa katika ngazi za juu za Serikali.

Mswada unaotarajiwa kuwasilishwa ni ahadi ya Serikali tangu mwaka 2007.  Serikali ipo tayari kupokea hoja mbalimbali baada ya kuwasilisha mswada huu Bungeni kwa maana ya kuboresha ikiwemo Haki ya Kupata Habari.

Serikali inawataka wadau wa habari na watanzania kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuhakikisha kwamba Mswada wa Kusimamia vyombo vya Habari unakamilika na kuwa sheria lengo likiwa ni kujenga misingi ya demokrasia na utawala bora.

24/1/2013

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO