Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAONI YA VYAMA VYA SIASA KATIBA MPYA: CHADEMA WATAKA UMRI WA URAIS USHUSHWE, CUF WALIA NA MUUNGANO WA MKATABA, CCM WABEBA LA MGOMBEA BINAFSI

Wajumbe wawakilishi wa CHADEMA wakiongozwa na Mwenyekiti Mh Mbowe, katika kikao cha pamoja na Tume ya Kukusanya Maoni ya Katiba Mpya jana Jijini Dar es Salaam wapipoenda kuwasilisha maoni yao. Picha na Tume ya Katiba

TUME ya Mabadiliko ya Katiba, jana ilianza kukusanya maoni ya vyama vya siasa katika mchakato wa Katiba Mpya, huku baadhi ya vyama hivyo vikitoa mapendekezo mbalimbali kuhusu suala la urais.

Vyama vilivyozungumzia urais katika mkutano huo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam ni CCM, CUF na Chadema.

Taarifa za vyama hivyo zilipatikana baada ya wawakilishi wao kuwasilisha maoni kwenye tume hiyo katika mkutano wa ndani ambao waandishi wa habari hawakuruhusiwa kuingia.

Wakati CCM ikitaka Katiba ijayo iruhusu mgombea binafsi, Chadema imependekeza Mtanzania yeyote mwenye umri wa kuanzia miaka 18 aruhusiwe kupiga kura na kugombea nafasi yeyote ya uongozi nchini. CUF imependekeza Muungano wa Mkataba.

Mwanasheria wa Chadema ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu alisema chama hicho cha upinzani, kimependekeza Katiba Mpya imtambue mtu mwenye umri wa kuanzia miaka 18 kuwa ana haki ya kuchagua na kuchaguliwa kushika nafasi yoyote ya uongozi nchini.

“Haingii akilini kwa mtu mwenye umri wa miaka 18 anakubalika kupiga kura na kumchagua kiongozi anayemtaka, lakini yeye mwenyewe hakubaliki kugombea nafasi yoyote ya uongozi ikiwamo urais, ubunge na udiwani,” alisema Lissu.

Alihoji “Kama Katiba ya sasa inamtambua mtu mzima kuwa ni yule anayeanzia umri wa miaka 18, kwa nini linapokuja suala la kuchaguliwa kwa ngazi zote ananyimwa haki hiyo hata kama ana vigezo vingine?”
Pia Lissu alisema kuwa Katiba Mpya haina budi kuanzisha utawala wa majimbo yasiyozidi kumi ili kuleta uwiano katika matumizi ya rasilimali kwenye maeneo yote ya nchi.

Aliyataja majimbo hayo kuwa ni Jimbo la Nyanza Magharibi ambalo litajumuisha mikoa ya Kagera, Geita na Shinyanga; Nyanza Mashariki mikoa ya Mwanza, Mara na Simiyu, Ziwa Tanganyika kwa mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa na Jimbo la Kati litakalojumuisha mikoa ya Dodoma, Tabora, Singida na Iringa.

Mengine na mikoa yake kwenye mabano ni Jimbo la Kaskazini ( Arusha, Manyara na Kilimanjaro), Pwani ya Kaskazini (Tanga, sehemu za Pwani na sehemu za Morogoro), Jimbo la Dar es Salaam, Jimbo la Pwani Kusini (Mtwara, Lindi, Wilaya za Mafia, Rufiji na Ulanga) na Kanda ya Nyanda za Juu (Njombe, Mbeya na Ruvuma).

Mwakilishi wa CCM, Andrew Chenge alipendekeza kuwapo kwa mgombea binafsi katika nafasi zote ili kutoa fursa ya wananchi wasio wanachama wa chama chochote cha siasa kupata nafasi ya uongozi.

Alisema, kitakachofanyika ni kitengeneza mazingira mazuri ambayo yatawezesha mgombea huyo kupatikana bila ya kuwapo kwa itikadi za udini au ukabila.

“Mapendekezo ya chama chetu ni kuwapo kwa mgombea binafsi ili kushiriki kwenye nafasi zote za uongozi. Hii itasaidia kuondoa ubaguzi au kuleta udini, jambo ambalo linaweza kutoa fursa kwa wananchi wasio na udini wala chama kushiriki kwenye nafasi ya uongozi,”alisema Chenge.

Chanzo: Mwananchi

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO