Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Kampeni ya Mama Ye! Yazinduliwa Arusha, Kampeni ya Uchangiaji Damu Kuokoa Maisha ya Mama na Mtoto Jijini Arusha leo

DSCN7322Jijini Arusha leo limefanyika zoezi la uchangiaji damu kwa hiari kwa ajili ya kusaidia kampeni ya kuokoa maisha ya mama  na mtoto inayoratibiwa na asasi za Evidence for Action(non governmental organisation) wakishirikiana na TRCS katika kuzindua kampeni ya Mama Ye! Zoezi hilo lilifanyika katika viwanja vya Makumbusho ya Azimio la Arusha ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Monduli, Mh Kasunga. “Changia Damu, Okoa Maisha ya Mama na Mtoto”Arusha. Jumla ya wachangiaji 1040 walijitolea damu.

DSCN7329Kaimu Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha, Mh Karimu akizungumza katika zoezi hilo lililofanyika katiba bustani ya Makumbusho ya Azimio la Arusha.

DSCN7326Mshereheshaji wa tukio zima, Bw Keneth Simbaye akiwajibika jukwaani

DSCN7316

DSCN7318Baadhi ya wananfunzi ambao wamekwishachangia damu wakiwa wamepumzishwa kivulini na wahudumu wa Mama Ye viwanjani hapo!

DSCN7323Wananfunzi ambao wako kwenye foleni ya kuchnagia damu

DSCN7320Mhudumu wa kampeni za Mama Ye! akiendelea na zoezi la kusaidia uchangiaji damu Jijini Arusha leo

DSCN7321Mhudumu wa Mama Ye! akimuandaa mwanafunzi kwa ajili ya uchangiaji damu

DSCN7314Mwanafunzi akipatiwa ushauri na kuchukuliwa maelezo ya kiafya kabla ya kuruhusiwa kuchangia damu ili kuokoa maisha ya mama na mtoto

DSCN7315Mhudumu akimuelekeza mama huyu mahali pa kwenda kutoa damu kwa ajili ya uchangiaji damu kwa hiyari Jijini Arusha leo, zoezi lililofanyika katika viwanja vya Makumbusho ya Azimio la Arusha chini ya uratibu wa taasisi ya Evidence for Action naTRCS !

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO