Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Rufaa ya Lema kusikilizwa leo

RUFAA ya kupinga kuvuliwa ubunge wa aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), inatarajiwa kusikilizwa leo na jopo la majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa, wakiongozwa na Jaji Mkuu wa Tanzania, Mohamed Chande.

Majaji wengine waliopo katika kusikiliza rufaa hiyo inayovuta hisia za watu wengi ni pamoja na Jaji Natalia Kimaro na Salum Massati, wote wa Mahakama ya Rufaa nchini.

Rufaa hiyo ambayo ilipaswa kusikilizwa Septemba 23, mwaka huu, ilisogezwa mbele hadi Oktoba 2, kutokana na mawakili wa pande zote mbili kupatwa na dharura, ambapo jopo hilo liliridhika na hivyo kusogeza mbele tarehe.

Jopo hilo lilizingatia barua iliyoomba kusogezwa mbele kwa shauri hilo hadi Oktoba 2, kutokana na mawakili, Tundu Lissu, anayemtetea Lema na kaka yake, Alute Mughwai, anayewatetea walalamikaji kufiwa na baba yao mzazi.

Tundu Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), anashirikiana na Wakili Mwandamizi Method Kimomogoro katika kumtetea mrufani, Godbless Lema.

Kwa upande wake Wakili Mughwai anashirikiana na Wakili Modest Akida kuwawakilisha wadaiwa katika shauri hilo ambao ni wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mussa Mkanga, Agness Mollel na Happy Kivuyo.

Wanachama hao walifungua shauri lililotengua ubunge wa Lema wakidai kuwa wakati wa kampeni alimdhalilisha aliyekuwa mgombea wa CCM, Dk. Batilda Burian, kwa kutumia lugha za matusi.

Awali, Lema kupitia wakili wake, Method Kimomogoro, anayesaidiana na Lissu, aliwasilisha katika mahakama hiyo hoja 18 za madai, akipinga ubunge wake kutenguliwa na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha Aprili 5, mwaka huu.

Katika baadhi ya madai hayo, Lema aliiomba Mahakama ya Rufaa kutengua uamuzi wa Mahakama Kuu, huku akiitaka mahakama hiyo imtangaze kuwa mbunge halali wa Jimbo la Arusha Mjini.

Aidha, aliitaka mahakama hiyo ya juu, iwaamuru walalamikiwa katika shauri hilo walipe gharama za rufaa hiyo pamoja na gharama za kesi iliyomalizika katika Mahakama Kuu Kanda ya Arusha.

Katika madai mengine, Lema anamlalamikia Jaji Gabriel Rwakibarila, aliyesikiliza kesi hiyo kuwa alitoa uamuzi wake kwa kuzingatia maneno ya uvumi, huku akipuuza ushahidi uliotolewa mahakamani hapo

Kwa msaada wa Gazeti la Mtanzania

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO