Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Bunge lalipuka tena, Zitto, Sugu, Lembeli waibua mapya

BUNGE la Muungano lililomaliza kikao chake cha kumi jana, lilitikisika baada ya kuibuka kwa tuhuma nyingine nzito zilizoelekezwa moja kwa moja kwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, na naibu wake, Adamu Malima, na Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige.

Wakati Ngeleja akishambuliwa kwa kusema uongo na kuficha ufisadi wa kutisha wa ubinafsishaji, Waziri Maige amekaangwa kwa tuhuma za kujihusisha katika ugawaji vitalu vya uwindaji kinyume na sheria.

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James lembeli, ndiye aliyeibua tuhuma hizo nzito, kiasi cha kuitaka serikali kumwajibisha waziri huyo, hatua ambayo imezidi kuonyesha uozo wa utendaji ndani ya serikali.

Read more……

Source: Tanzania Daima 24th April, 2012

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO