Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Waziri Mkuu Pinda Atembelea Kiwanda cha nguo, Sun Flag (A to Z) cha Arusha

IMG_8950-- Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua  utengenezaji  vyandarua na nguo katika kiwanda cha A to Z cha Arusha Aprili 15,2012. Kushoto ni Mtendaji Mkuu wa kwanda hicho,  Anuj Shah. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa hisani ya Daily Mitikas Blog)

Waziri Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Mizengo Kayanza Peter Pinda, leo alifanya ziara katika kiwanda cha nguo cha Sun Flag kilichoko eneo la viwanda Themi, Jijini Arusha.

Katika hotuba yake, mara baada ya matembezi kuangalia jinsi uzalishaji wa nguo na vitambaa unavyofanyika kiwandani hapo Waziri Mkuu alisema Serikali itaviwezesha viwanda vya nguo vya ndani ili viweze kuzalisha kwa ufanisi zaidi.

Sunflag (Tanzania) Limited ilianzishwa mwaka 1965 na kwa sasa imeajiri zaidi ya watu 2700 kutoka nyanja zote za maisha.

Jiwe la msingi la kiwanda hiki liliwekwa mapema miaka ya 1930 na Mwenyekiti wa Sunflag Group, Bw. Satya Dev Bhardwaj, wakati alipoanzisha kiwanda cha kwanza nchini Kenya.

Hadi kufikia leo, Sunflag Group wanafanya kazi za uzalishaji nguo sehemu mbalimbali duniani kupitia ofisi na viwanda vyao vilivyoko  United Kingdom, India, Thailand, Kenya, Nigeria, USA na hapa  nyumbani Tanzania.

maelezo ya ziada yamepatikana kwenye website ya kiwanda

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO