Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

News Alert: Katibu Mwenezi wa Vijana Wilaya ya Londigo (CCM) nae Ajiengua CCM

Baada ya aliekuwa Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha, James Ole Millya kujiengua chama hicho na kutangaza kujiunga na CHADEMA juzi, jana Katibu Mwenezi wa Vijana Wilaya ya Longido iliyoko Mkoani Arusha pia, Ndg Yohana Laizer nae ameamua kukihama chama chake cha CCM lakini  bado hajaweka wazi atajiunga na chama gani.

Lakini taarifa zinaeleza kuwa kuna uwezekano mkubwa kwa Laizer kuungana na Millya ambae ameamua kujiunga na CHADEMA.

Taarifa hizo zinaeleza kua uamuzi wa Katibu huyo Mwenezi unatokana na madai yake ya kuchoshwa na viongozi wa CCM kuchanganya siasa na mila kiasi kwamba imefikia mahali wanawatishia Wamasai kutojiunga na vyama vya upinzani.

Blog hii imepokea taarifa hizi kutoka vyanzo vyake vya kuaminika, lakini bado inaendelea kufuatilia usahihi wake…..

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO