Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Vijana wa ‘bodaboda’ walionyongwa Arusha wadaiwa walikuwa wezi

WATU wanne wanaosadikiwa kuwa ni madereva wa pikipiki maarufu bodaboda ambao waliuawa kwa kunyongwa kisha kuvunjwa shingo na watu wasiotambulika usiku wa kuamkia juzi wilayani Arumeru mkoani Arusha, inadaiwa kuwa ni wezi waliokuwa wakisumbua katika Kata ya Sombetini ndani ya Jiji la Arusha.

Kuuawa kwa watu hao kumethibitishwa na Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye na maiti zao ziko katika chumba cha kuhifadhi maiti katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru.

Habari kutoka kwa wakazi wa Sombetini zilidai kuwa mpango mkali uliandaliwa kuwasaka wezi hao ambao hufanya kazi ya kuendesha bodaboda kama kisingizio, lakini ikifika saa 6 hadi 8 usiku, hufanya kazi ya kuvunja nyumba Sombetini na Nguselo.

Mmoja wa watoa habari aliyekataa kutajwa jina gazetini, alidai kuwa mpango huo ulisukwa
kimyakimya kwa kuhusisha watu wachache wa Sombetini, wa kuwasaka kila walipokuwa wakifanya kazi yao ya bodaboda.

Vyanzo vingine vilieleza kuwa bado kuna mwizi mmoja ambaye ni kiongozi wa waliouawa, anatafutwa na watu hao wa Sombetini ili apate kile walichopata wenzake kwani ndiye mfadhili mkubwa wa ujambazi.

Maiti hizo zilikutwa zikiwa na kamba za katani shingoni, mikononi na minyororo shingoni na mikononi ambayo inasadikiwa kutumika kuwafunga watu hao kabla ya kuwanyonga, hali inayoonesha kuwa kulikuwa na purukushani kabla ya kunyongwa kwao.

Baadhi ya watu waliofika kutambua miili hiyo, waliitambua mitatu kati ya minne ambayo ni Jumbe Saitobi, Elly Lotti, Boshu Maombi; wote ni wakazi wa Arusha na wanakadiriwa kuwa na umri kati ya miaka 30-35.

CHANZO: Habari Leo

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO