Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Zitto asikitishwa na rushwa kwa wabunge kuelekea uchaguzi wa wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki

zitto Katika ukurasa wake wa Facebook hii leo, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo ambae pia ni Mbunge wa Bunge la jamhuri ya Muungano, Mh Zitto Kabwe ameelezea kusikitishwa kwake na vitendo vya rushwa ya wazi kabisa kwa wabuge ili kuchagua wagombea fulani kwa uwakishili wa nchi katika Bunge la Afrika Mashariki, uchaguzi uliokuwa uanatarajiwa kufanyika April 17,2012.

Tayari kuna ombi la CHADEMA liliotumwa juzi likimtaka Spika wa Bunge, Mh Anne Makinda kusogeza mbele tarehe ya uchaguzi huo ili kuweka sawa taratibu fulani ambazo zimeonekeana kama zimekiukwa kwa mujibu wa Mkataba wa Shirikisho la Afrika Mashariki, jambo ambalo limeonekana kubana uhuru wa kidemokrasia kwa wananchi kupata uwakilishi unaowastahili.

Zitto ameonesha masikitiko yake kiasi cha kuamua kuibatiza Tanzania kama “The Land of The Corrupt” aka “FISADISTAN” kutokana na kukithiri kwake kwa vitendo vya rushwa.

Bandiko lake kupitia' akaunti yake ya ‘Facebook’ limesomeka hivi "Rushwa inavyotembezwa katika uchaguzi wa Wabunge wa Afrika Mashariki inatia simanzi sana. Haingii akilini kwangu kabisa kwamba Mbunge anahongwa ili kuchagua Mgombea fulani. Nchi hii inanuka uvundo. Uvundo wa Ufisadi. Sasa ni sahihi nchi hii kubatizwa jina jipya FISADISTAN 'The Land of The Corrupt'"

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO