Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Zilizotufikia Sasa Hivi: Ndege Ya ATCL Yaanguka Kigoma

Ndege ya shirika la ATCL imeanguka mkoani Kigoma baada ya kushindwa kuruka wakati ikianza safari yake kuelekea Tabora na Dar es Salaam. Inaelezwa kuwa ndege hiyo imeharibika vibaya, na taarifa za uhakika zinasema kwamba hakuna abiria yeyote aliyeumia sana. Jumla ya abiria 41 wamenusurika kifo katika ajali hiyo na utaratibu wa kuwasafirisha abiria na majeruhi unafanywa jijini Dar es Salaam.

Atc1Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATC), aina ya Dash 8-300 iliyokuwa inatoka Kigoma kwenda Dar es Salaam kupitia Tabora, ikiwa imeanguka jana baada ya kuteleza kutokana na tope jingi kuwepo kwenye njia ya kurukia ya Uwanja wa Ndege wa Kigoma. Abiria 35 na wafanyakazi wanne walinusurika kwenye ajali hiyo

atc2Hali ya ndege inavyoonekana upande wa kushoto

Atc3Wananchi wakiangalia ajali ya ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATC), aina ya Dash 8-300 iliyokuwa inatoka Kigoma kwenda Dar es Salaam kupitia Tabora, ikiwa imeanguka jana baada ya kuteleza kutokana na tope jingi kuwepo kwenye njia ya kurukia ya Uwanja wa Ndege wa Kigoma. Abiria 35 na wafanyakazi wanne walinusurika kwenye ajali hiyo

atc4    Hali ilivyokuwa inaonekana ndani ya ndege baada ya ajali kutokea jana katika Uwanja wa Ndege wa Kigoma.

Source: Mjengwa BLOG

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO