Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MAMIA WAJITOKEZA KUMPOKEA PROF LIPUMBA

mapokezi ya prof lipumba Mamia ya wakazi wa Dar es Slaam na maeneo ya jirani, wengi wakiwa ni wafuasi wa chama cha CUF, leo wamejitokeza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius K Nyerere kumlaki Mwenyekiti wa  chama hicho, Prof. Ibrahim Lipumba akirejea nyumbani toka Marekani alikokuwa kwa zaidi ya miezi 5.

Hivi karibuni, Prof. Lipumba alichaguliwa na jopo la wachumi wa dunia kuwa mwenyekiti  wao,  nafasi ambayo ameipata kutokana na ujuzi, uzoefu, na elimu aliyonayo katika maswala mambo ya Uchumi.

Akizungumza uwanjani hapo mara baada ya kuwasili, Prof Lipumba alisema kuwa katika mambo aliyotokanayo Marekani ni pamoja na ukweli kwamb uchumi shirikishi na demokrasia, sambamba na utawala bora unaowajibika kwa wananchi ndio nyenzo kuu kwa Bara la Afrika katika kupambana naumasikini.

Alipohitajika kuzungumzia fukuto la migogoro ndani ya chama chake, aliahidi kulitolea majibu swala hilo kesho.

Maandalizi ya mapokezi ya Mwenyekiti huyu wa wachumi Duniani yaliratibiwa kwa sehemu kubwa na chama cha CUF ambapo msafara wake ulielezwa kutakiwa kupita Barabara ya Nyerere, Mandela, Morogoro, Msimbazi, Uhuru, hadi viwanja vya Karume.


Picha: Mjengwa Blog
Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO