Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

News Alert: Virajilal Jitu Son (CCM) Ashinda Kesi ya Kupinga Ubunge wake Babati Vijijini

Hatma ya Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini (CCM), Virajilal Jitu Son imefahamika leo baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kutoa hukumu ya kesi ya kupinga ubunge wake iliyofunguliwa na aliyegombea ubunge wa Jimbo hilo, Laurence Sharubu Tara (NCCR Mageuzi)

Mahakama imemruhusu Jitu Son kuendelea na Ubunge wake na kutupilia mbali maombi ya Tara, ambaye ni Diwani wa Kata ya Bashnet ya kuitaka Mahakama hiyo imtangaze kuwa Mbunge halali akidai kuwa alimshinda Jitu Son kwa tofauti ya kura 58.

Kesi hiyo namba 12/2010 ilikuwa ikisikilizwa na Jaji Fatuma Massengi na ilifunguliwa Novemba 2010 na kuanza kusikilizwa February 16 mwaka huu huku wadaiwa wakiwa ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo hilo na Mh Jitu Son.

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO