Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

MKUTANO WA KAMPENI CHADEMA, TENGERU STAND LEO MACHI 17

Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, CHADEMA leo kimefanya mikutano mitatu kama ilivyo ratiba yake ya kila siku kwa kamapeni za uchaguzi mdogo Jimbo la Arumeru Mashariki. Hii ni mbali na kampeni nyingine za nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa zinazoendelea Jimboni humo.

Siku ya leo walifanya mkutano wa kwanza Kikatiti na wa pili eneo la Nkoaranga Wilayani Arumeru, na mkutano wa mwisho ulifanyika eneo la stand mpya ya mabasi/vifodi eneo la Tengeru.

Mgombea wa chama hicho aliweza kuhutubia mkutano wa kwanza na wa pili lakini hakuweza kupatikana kwa mkutano wa tatu Tengeru kutokana na mabadiliko ya ghafla katika ratiba yake ya kampeni.

Pamoja na kutokuwepo kwa Nassari, bado mkutano wa Tengeru uliweza kufanyika kwa ufasisi mkubwa chini ya usimamizi na uhamasishaji wa Waitara Mwita Mwikabwe, Mch Msigwa na Mbunge wa Viti Maalumu Moshi, Mh Grace Kiwhelu, ambao ndio pekee waliohutubia mamaia ya watu waliojitokeza, sambamba na diwani mmoja wa viti maalumu kutoka Arusha Mjini.

Hali ya usalama ilikuwa ni tulivu sana na ya kutia matumaini, hakukuwa na kashkashi yoyote ile na mwisho mkutano ukamalizwa ndani ya muda uliokubaliwa. Picha chache zifuatazo zinaweza kuwa na maelezo zaidi…

DSCN9981Sehemu ya umati uliojitokeza uwanjani hapo leo..

DSCN9989Mchungaji Peter Msigwa, ambae pia ni Mbunge wa Iringa Mjini akihutubia

Wananchi wakishiriki ishara ya “Peoples Power” 

DSCN0021Miselebuko nayo haikukosekana baada ya mkutano kuisha

DSCN0018Huyu dogo alikuwa kivutio sana…. Alipandishwa jukwani na kusalimia 

DSCN9991Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Monduli, Aman Ole Silanda (mwenye kofia) aka “mwarobaini wa Lowassa” alikuwepo uwanjani.
Ndie aliyekuwa mpinzani Mkuu wa Lowassa katika Uchaguzi wa 2010

Kamanda Mwikabwe Mwita Waitara akishuka jukwaani

DSCN0030Wamama hawa pamoja na kuwa busy na biashara hawakusita kushangilia msafara wa viongozi wa CHADEMA uliokuwa ukipita mbele yao baada ya mkutano kuisha

DSCN0011 Hamasa ilikuwa kubwa sana…

DSCN9979Jukwaa kuu halikuwa na wale wabunge machachari waliozoeleka…

DSCN0015 Zoezi la uchangishaji ‘sadaka’ lilipita mpaka nje ya mkusanyiko, hadi kwenye mapumzikio ya abiria stand

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

1 maoni:

Kiu ya Haki said...

Ushindi upo upande wetu, Pipoz.....

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO