Tunakusogezea karibu habari na matukio, zaidi habari za kisiasa na utawala, matukio ya Arusha na maeneo jirani, bila kusahau na mambo mengineyo ya kitaifa yanayojiri katika maeneo mbalimbali ya nchi kuhusu maendeleo na kuwa ya maslahi kwa watu wengi. Burudani na michezo pia havijasahaulika. Kizuri zaidi, unaweza kupata link ya Blogu nyingine na website muhimu hapa hapa kwa kuscroll mpaka chini. Karibu tuhabarike!

Kampeni ya CHADEMA Arumeru, Machi 22

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) jana kilianza kutumia helkopta rasmi katika kampeni zake za kumnadi mgombea wake wa ubunge katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassa.

Mara ya mwisho kutumia chombo hicho ilkuwa ni Machi 10 wakati wa ufunguzi wa kampeni.

Mkuu wa Operesheni wa uchaguzi wa Chadema katika jimbo hilo, John Mrema anasema kuanza kutumika kwa helkopta hiyo kutamwezesha mgombea wao kufanya mikutano mitano hadi nane kwenye kata tano tofauti kwa siku.

Mikutano ya jana ilifanyika katika vijiji vya Ngurdoto Kata ya Maji ya Chai, Ngabobo Kata ya Ngarenanyuki, Kijiji cha Sakila Kata ya Kikatiti na vijiji na kata za King’ori na Nkoanrua.

Katika mkutano wa Kata ya Ngarenanyuki, mgombea wa CHADEMA, Joshua Nassari alichinjiwa ng’ombe wanne na kuvalishwa mgolole sambamba na kukabidhiwa rungu la Kimasai.

helchedemaMgombea wa CHADEMA, Joshua Nassari akisalimia wananchi mara baada ya kuwasili uwanjani kati ya moja ya mikutano yake jirani na Sing’isi

Dr Slaa akimnadi mgombea wa chama chake

DSCN0221Wananchi wakifuatilia kampeni

DSCN0217Karibia kampeni zote, CHADEMA wamekuwa wakitumia magari yao mawili maalumu kwa matangzao ambayoyana jukwaa na PA System, Generator na kila kitu hapo hapo.

DSCN0218

Washirikishe Google Plus

About SeriaJr

SeriaJr will keep you updated with all current political news countrywide "Ndiye "Bosi" Mzito Arusha255" Karibu Tuhabarike!.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 maoni:

TANZANIA, THE HOME OF KILIMANJARO